Na *Patrick Roman*
Napenda kukuandikia.
Ni katika pitapita nakutana na mfugaji huko Ethiopia jina lake ni Kaamila,n mama wa watoto kadhaa,mfugaji mdogo.
Nchini Ethiopia hichi ni kipindi cha kiangazi chenye ukame mkubwa unaomlazimu mfugaji huyu kutafuta malisho kwaajili ya ng'ombe wake.
Anasema kuwa katika kipindi kama hichi yeye huamua kutembea umbali wa siku 3 hadi katika maeneo ya milima ili kupata maeneo ya malisho kulisha ng'ombe wake.Watoto wake hulazimika kutoenda shule kwa muda wote wa ukame ili waandamane na mama yao, kwa kuwa hakuna wa kubaki nyumbani.
"Ni kipindi kigumu sana kwangu,familia,na mifugo yangu,tunalala katika vichaka,tunatembea umbali mrefu ili kuhakikisha tunapata malisho" anasema Kaamila
Kaamila ni miongoni mwa wafugaji na wakulima wanaopitia halingumu Afrika. Bado hawajanufaika na Kazi zao, mabadiliko ya teknolojia hayajawagusa.
Hali kama za Kaamila ndizo zinazopelekea kukata tamaa kwa wengi wetu katika maswala ya Kilimo na Ufugaji.
Wewe unamaoni gani katika kurudisha hamasa na kutatua changamoto hzi????????
Kumbuka:������������
Green Tanzania Youth Movement,COMING SOON!��������
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni